Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 4:14-29 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Yerusalemu, yasafishe maovu moyoni mwako,ili upate kuokolewa.Mpaka lini utaendelea kuwaza maovu?

15. Sauti kutoka Dani inatoa taarifa;inatangaza maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16. Inayaonya mataifa,inaitangazia Yerusalemu:“Wavamizi waja kutoka nchi ya mbali,wanaitisha miji ya Yuda,

17. wanauzingira Yerusalemu kama walinda mashamba,kwa sababu watu wake wameniasi mimi Mwenyezi-Mungu.

18. Yuda, mwenendo wako na matendo yako yamekuletea hayo.Hayo ndiyo maafa yaliyokupata, tena ni machungu;yamepenya mpaka ndani moyoni mwako.”

19. Uchungu, uchungu!Nagaagaa kwa uchungu!Moyo wangu unanigonga vibaya.Wala siwezi kukaa kimya.Maana naogopa mlio wa tarumbeta,nasikia kingora cha vita.

20. Maafa baada ya maafa,nchi yote imeharibiwa.Ghafla makazi yangu yameharibiwa,na hata mapazia yake kwa dakika moja.

21. Hadi lini nitaona bendera ya vitana kuisikia sauti ya tarumbeta?

22. Mwenyezi-Mungu asema:“Watu wangu ni wapumbavu,hawanijui mimi.Wao ni watoto wajinga;hawaelewi kitu chochote.Ni mabingwa sana wa kutenda maovu,wala hawajui kutenda mema.”

23. Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.

24. Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.

25. Nilikodoa macho wala sikuona mtu;hata ndege angani walikuwa wametoweka.

26. Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,na miji yake yote imekuwa magofu matupu,kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.

27. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nchi nzima itakuwa jangwa tupu;lakini sitaiharibu kabisa.

28. Kwa hiyo, nchi itaomboleza,na mbingu zitakuwa nyeusi.Maana, nimetamka na sitabadili nia yangu;nimeamua, wala sitarudi nyuma.

29. Watakaposikika wapandafarasi na wapiga mishale,kila mmoja atatimua mbio.Baadhi yao watakimbilia msituni,wengine watapanda majabali.Kila mji utaachwa tupu;hakuna mtu atakayekaa ndani.

Kusoma sura kamili Yeremia 4