Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Watarudi wakiwa wanatoa machozi,nitawarudisha nikiwafariji;nitawapitisha kando ya vijito vya maji,katika njia iliyonyoka ambamo hawatajikwaa;maana mimi nimekuwa baba wa Israeli,Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.

10. Enyi mataifa, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu,litangazeni katika nchi za mbali,semeni: ‘Aliyemtawanya Israeli, atamkusanya,atamtunza kama mchungaji atunzavyo kondoo wake.’

11. Maana mimi Mwenyezi-Mungu nimemkomboa Yakobo,nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.

12. Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mlima Siyoni,wataona fahari juu ya wema wangu mimi Mwenyezi-Mungu,kwa nafaka, divai na mafuta niwapavyo,kwa kondoo na ng'ombe kadhalika;maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji,wala hawatadhoofika tena.

13. Ndipo wasichana wao watafurahi na kucheza,vijana na wazee watashangilia kwa furaha.Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha,nitawafariji na kuwapa furaha badala ya huzuni.

14. Nitawashibisha makuhani kwa vinono,nitawaridhisha watu wangu kwa wema wangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

15. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sauti imesikika mjini Rama,maombolezo na kilio cha uchungu.Raheli anawalilia watoto wake,wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao,maana wote hawako tena.

16. Sasa, acha kulia,futa machozi yako,kwani utapata tuzo kwa kazi yako,mimi Mwenyezi-Mungu nimesema;watoto wenu watarudi kutoka nchi ya maadui zenu.

17. Yapo matumaini kwa siku zenu zijazo,mimi Mwenyezi-Mungu nimesema;kwani watoto wenu watarejea nchini mwao.

Kusoma sura kamili Yeremia 31