Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:14-19 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Nitawashibisha makuhani kwa vinono,nitawaridhisha watu wangu kwa wema wangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

15. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sauti imesikika mjini Rama,maombolezo na kilio cha uchungu.Raheli anawalilia watoto wake,wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao,maana wote hawako tena.

16. Sasa, acha kulia,futa machozi yako,kwani utapata tuzo kwa kazi yako,mimi Mwenyezi-Mungu nimesema;watoto wenu watarudi kutoka nchi ya maadui zenu.

17. Yapo matumaini kwa siku zenu zijazo,mimi Mwenyezi-Mungu nimesema;kwani watoto wenu watarejea nchini mwao.

18. “Nimesikia Efraimu akilalamika:‘Umenichapa ukanifunza nidhamu,kwani nilikuwa kama ndama asiyezoea nira.Unigeuze nami nitakugeukia,kwani wewe ndiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.

19. Maana baada ya kukuasi, nilitubu,na baada ya kufunzwa, nilijilaumu,nikaona haya na kuaibika,maana lawama za ujana wangu ziliniandama.’

Kusoma sura kamili Yeremia 31