Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu asema: “Wakati utakuja ambapo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli nao watakuwa watu wangu.

2. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Watu walionusurika kuuawaniliwaneemesha jangwani.Wakati Israeli alipotafuta kupumzika,

3. mimi Mwenyezi-Mungu nilimtokea kwa mbali.Nami nimekupenda kwa mapendo ya daima,kwa hiyo nimeendelea kuwa mwaminifu kwako.

4. Nitakujenga upya nawe utajengeka,ewe Israeli uliye mzuri!Utazichukua tena ngoma zakoucheze kwa furaha na shangwe.

5. Utapanda tena mizabibujuu ya milima ya Samaria;wakulima watapanda mbeguna kuyafurahia mazao yake!

6. Maana siku yaja ambapo mlinzi atapiga mbiukatika vilima vya Efraimu:‘Amkeni, twende juu mpaka Siyonikwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.’”

7. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Imbeni kwa furaha kwa ajili ya Yakobo,pigeni vigelegele kwa ajili ya taifa kuu,tangazeni, shangilieni na kusema:‘Mwenyezi-Mungu na awaokoe watu wake,amewaletea ukombozi waliobaki wa Israeli!’

8. Tazama, nitawaleta kutoka nchi ya kaskazini,nitawakusanya kutoka miisho ya dunia.Wote watakuwapo hapo;hata vipofu na vilema,wanawake waja wazito na wanaojifungua;umati mkubwa sana utarudi hapa.

Kusoma sura kamili Yeremia 31