Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 2:29-37 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Mbona mnanilalamikia?Nyinyi nyote mmeniasi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

30. Niliwaadhibu watu wako bila kufanikiwa,wao wenyewe walikataa kukosolewa.Upanga wako uliwamaliza manabii wakokama simba mwenye uchu.

31. Enyi watu! Sikilizeni ninachosema mimi Mwenyezi-Mungu:Je, nimekuwa jangwa kwa Israeliau nchi yenye giza nene?Kwa nini basi watu wangu waseme:‘Sisi tu watu huru;hatutakuja kwako tena!’

32. Kijana msichana aweza kusahau mapambo yakeau bibi arusi mavazi yake?Lakini watu wangu wamenisahaukwa muda wa siku zisizohesabika.

33. Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi!Hata wanawake wabaya huwafundisha njia zako.

34. Nguo zako zina damu ya maskini wasio na hatia,japo hukuwakuta wakivunja nyumba yako.“Lakini licha ya hayo yote,

35. wewe wasema: ‘Mimi sina hatia;hakika hasira yake imegeuka mbali nami.’Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema:‘Sikutenda dhambi.’

36. Kwa nini unajirahisisha hivi,ukibadilibadili mwenendo wako?Utaaibishwa na Misri,kama ulivyoaibishwa na Ashuru.

37. Na huko pia utatoka,mikono kichwani kwa aibu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimewakataa wale uliowategemea,wala hutafanikiwa kwa msaada wao.

Kusoma sura kamili Yeremia 2