Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 2:14-30 Biblia Habari Njema (BHN)

14. “Je, Israeli ni mtumwa,ama amezaliwa utumwani?Mbona basi amekuwa kama mawindo?

15. Simba wanamngurumia,wananguruma kwa sauti kubwa.Nchi yake wameifanya jangwa,miji yake imekuwa magofu, haina watu.

16. Isitoshe, watu wa Memfisi na Tahpanesi,wameuvunja utosi wake.

17. Israeli, je, hayo yote si umejiletea mwenyewe,kwa kuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,niliyekuwa ninakuongoza njiani?

18. Na sasa itakufaa nini kwenda Misri,kunywa maji ya mto Nili?Au itakufaa nini kwenda Ashuru,kunywa maji ya mto Eufrate?

19. Uovu wako utakuadhibu;na uasi wako utakuhukumu.Ujue na kutambua kuwa ni vibaya mnokuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,na kuondoa uchaji wangu ndani yako.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.

20. “Tangu zamani wewe ulivunja nira yako,ukaikatilia mbali minyororo yako,ukasema, ‘Sitakutumikia’.Juu ya kila kilima kirefuna chini ya kila mti wa majani mabichi,uliinamia miungu ya rutuba kama kahaba.

21. Lakini mimi nilikupanda kama mzabibu mteule,mzabibu wenye afya na wa mbegu safi;mbona basi umeharibika,ukageuka kuwa mzabibu mwitu?

22. Hata ukijiosha kwa magadi,na kutumia sabuni nyingi,madoa ya uovu wako bado yatabaki mbele yangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

23. “Unawezaje kusema, ‘Mimi si najisi;sijawafuata Mabaali?’Tazama ulivyotenda dhambi kule bondeni;angalia ulivyofanya huko!Wewe ni kama mtamba wa ngamia,akimbiaye huko na huko;

24. kama pundamwitu aliyezoea jangwani.Katika tamaa yake hunusanusa upepo;nani awezaye kuizuia hamu yake?Amtakaye hana haja ya kujisumbua;wakati wake ufikapo watampata tu.

25. Israeli, usiichakaze miguu yakowala usilikaushe koo lako.Lakini wewe wasema: ‘Hakuna tumaini lolote.Nimeipenda miungu ya kigeni,hiyo ndiyo nitakayoifuata.’

26. “Kama vile mwizi aonavyo aibu akishikwa,ndivyo Waisraeli watakavyoona aibu;wao wenyewe, wafalme wao, wakuu wao,makuhani wao na manabii wao.

27. Hao huuambia mti: ‘Wewe u baba yangu,’na jiwe: ‘Wewe ndiwe uliyenizaa;’kwa maana wamenipa kisogo,wala hawakunielekezea nyuso zao.Lakini wakati wa shida husema: ‘Inuka utuokoe!’

28. “Lakini iko wapi miungu yako uliyojifanyia?Iinuke basi, kama inaweza kukusaidia,wakati unapokuwa katika shida.Ee Yuda, idadi ya miungu yakoni sawa na idadi ya miji yako!

29. Mbona mnanilalamikia?Nyinyi nyote mmeniasi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

30. Niliwaadhibu watu wako bila kufanikiwa,wao wenyewe walikataa kukosolewa.Upanga wako uliwamaliza manabii wakokama simba mwenye uchu.

Kusoma sura kamili Yeremia 2