Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 18:12-19 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Lakini wao watasema, ‘Hiyo ni bure tu! Tutafuata mipango yetu wenyewe na kila mmoja wetu atafanya kwa kiburi kadiri ya moyo wake mwovu.’”

13. Basi, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Yaulize mataifa yote:Nani amewahi kusikia jambo kama hili.Israeli amefanya jambo la kuchukiza mno.

14. Je, majabali ya Lebanoni hukosa theluji?Je, vijito vya maji vya milima yake hukauka?

15. Lakini watu wangu wamenisahau mimi,wanafukizia ubani miungu ya uongo.Wamejikwaa katika njia zao,katika barabara za zamani.Wanapitia vichochoroni badala ya njia kuu.

16. Wameifanya nchi yao kuwa kitisho,kitu cha kuzomewa daima.Kila mtu apitaye huko hushangaana kutikisa kichwa chake.

17. Nitawatawanya mbele ya adui,kama upepo utokao mashariki.Nitawapa kisogo badala ya kuwaonesha uso wangusiku hiyo ya kupata maafa yao.”

18. Kisha, watu wakasema: “Njoni tumfanyie Yeremia njama, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha, wenye hekima wa kutushauri na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Njoni tumshtaki kwa maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maanani yote asemayo.”

19. Basi, mimi nikasali:Nitegee sikio ee Mwenyezi-Mungu,usikilize ombi langu.

Kusoma sura kamili Yeremia 18