Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 13:14-17 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Nitawagonganisha wao kwa wao kina baba na watoto. Sitawahurumia, sitawaachia wala sitawarehemu, bali nitawaangamiza.”

15. Enyi Waisraeli, sikilizeni kwa makini,msiwe na majivuno maana Mwenyezi-Mungu anasema nanyi.

16. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,kabla hajawaletea giza,nanyi mkajikwaa miguu kwenye milima ya giza.Nyinyi mnatazamia mwanga,lakini anaugeuza kuwa utusitusina kuufanya kuwa giza nene.

17. Lakini kama msiponisikiliza,moyo wangu utalia machozi faraghani,kwa sababu ya kiburi chenu.Nitalia kwa uchungu na kububujika machozi,kwa kuwa watu wa Mwenyezi-Mungu wametekwa.

Kusoma sura kamili Yeremia 13