6. Tazama ulivyo mzuri na wa kuvutia!Ewe mpenzi, mwali upendezaye!
7. Umbo lako lapendeza kama mtende,matiti yako ni kama shada za tende.
8. Nilisema nitaupanda mtende na kuzichuma shada za tende.Kwangu matiti yako ni kama shada za zabibu,harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matofaa;
9. na kinywa chako ni kama divai tamu.Basi divai na itiririke hadi kwa mpenzi wangu,ipite juu ya midomo yake na meno yake!
10. Mimi ni wake mpenzi wangu,naye anionea sana shauku.