Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 5:3-15 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Nimekwisha yavua mavazi yangu,nitayavaaje tena?Nimekwisha nawa miguu yangu,niichafueje tena?

4. Hapo mpenzi wangu akaugusa mlango,moyo wangu ukajaa furaha.

5. Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu.Mikono yangu imejaa manemane,na vidole vyangu vyadondosha manemane,nilipolishika komeo kufungua mlango.

6. Nilimfungulia mlango mpenzi wangu,lakini kumbe, alikuwa amekwisha toweka.Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumza!Nilimtafuta, lakini sikumpata;nilimwita, lakini hakuniitikia.

7. Walinzi wa mji waliniona,walipokuwa wanazunguka mjini;wakanipiga na kunijeruhi;nao walinzi wa lango wakaninyanganya shela langu.

8. Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,mkimwona mpenzi wangu,mwelezeni kwamba naugua kwa mapenzi!

9. Ewe upendezaye kuliko wanawake wote!Kwani huyo mpenzi wako ana nini cha zaidi ya mpenzi mwingine,hata utusihi kwa moyo kiasi hicho?

10. Mpenzi wangu ni mzuri na mwenye nguvu,mashuhuri miongoni mwa wanaume elfu kumi.

11. Kichwa chake kizuri kama dhahabu safi,nywele zake ni za ukoka,nyeusi ti kama kunguru.

12. Macho yake ni kama ya hua kandokando ya kijito,ni kama njiwa waliooga maziwa kando ya kijito.

13. Mashavu yake ni kama matuta ya rihanikama bustani iliyojaa manukato na manemane.Midomo yake ni kama yungiyungi,imelowa manemane kwa wingi.

14. Mikono yake imewekwa bangili za dhahabu,amevalia johari za Tarshishi.Kiwiliwili chake ni kama pembe za ndovuzilizopambwa kwa vito vya johari ya rangi ya samawati.

15. Miguu yake ni kama nguzo za alabastazilizosimikwa katika misingi ya dhahabu.Umbo lake ni kama Lebanoni,ni bora kama miti ya mierezi.

Kusoma sura kamili Wimbo Ulio Bora 5