Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 1:11-17 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Lakini tutakufanyizia mikufu ya dhahabu,iliyopambwa barabara kwa fedha.

12. Mfalme alipokuwa kwenye kochi lake,marashi yangu ya nardo yalisambaa kila mahali.

13. Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane kwangu,kati ya matiti yangu.

14. Mpenzi wangu ni kama maua ya hina yachanuayo,kwenye mashamba ya mizabibu huko Engedi.

15. Hakika u mzuri, ee mpenzi wangu,hakika u mzuri!Macho yako ni kama ya hua!

16. Hakika u mzuri ewe nikupendaye,u mzuri kweli!Majani mabichi yatakuwa kitanda chetu;

17. mierezi itakuwa nguzo za nyumba yetu,na miberoshi itakuwa dari yake.

Kusoma sura kamili Wimbo Ulio Bora 1