Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 25:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. “Katika mwaka huo chochote ambacho kiliuzwa ni lazima kirudishwe kwa mwenyewe.

14. Unaponunua au kuuza ardhi kwa jirani usimpunje.

15. Bei ya ardhi ni lazima ilingane na miaka kabla ya kurudishwa kwa mwenyewe.

16. Kama miaka inayohusika ni mingi utaongeza bei na kama miaka hiyo ni michache utapunguza bei, kwani bei yake itapimwa kulingana na mazao anayokuuzia.

17. Msipunjane, bali, mtamcha Mungu wenu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.

18. “Kwa hiyo, mtafuata masharti yangu na kutekeleza maagizo yangu, ili mpate kuendelea kuishi kwa usalama katika nchi.

Kusoma sura kamili Walawi 25