Agano la Kale

Agano Jipya

Walawi 13:50-58 Biblia Habari Njema (BHN)

50. Kuhani atauangalia upele huo na kuliweka vazi hilo kando kwa muda wa siku saba.

51. Siku ya saba atauangalia upele huo. Ikiwa upele huo umeenea katika vazi hilo, liwe ni la kufuma au kusokotwa au la ngozi au la ngozi ya aina yoyote ile, vazi hilo lina upele. Hivyo vazi hilo ni najisi.

52. Kuhani atalichoma moto vazi hilo kwani lina namna ya upele wa ukoma.

53. “Kama kuhani ataona kuwa upele haukuenea katika vazi, basi,

54. ataamuru vazi hilo lifuliwe na kuwekwa kando kwa muda mwingine wa siku saba.

55. Kuhani ataliangalia hilo vazi baada ya kuoshwa. Ikiwa ile alama haijabadilika rangi yake hata ingawa upele haukuenea, basi, vazi hilo ni najisi. Vazi hilo utalichoma moto, iwe alama ya upele ipo nyuma au mbele ya vazi hilo.

56. “Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kufuliwa, basi atararua ile sehemu iliyo na namna ya upele wa ukoma.

57. Kisha, ikiwa hiyo alama inaonekana tena baadaye katika vazi lililofumwa au lililosokotwa au katika kitu chochote cha ngozi, basi upele umeenea. Hapo vazi hilo utalichoma moto.

58. Lakini vazi ambalo upele umetokea baada ya kulifua itabidi lifuliwe mara ya pili na hivyo lipate kuwa safi.”

Kusoma sura kamili Walawi 13