Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:9-15 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Nawapa heshima makamanda wa Israeliwaliojitoa kwa hiari yao kati ya watu.Mshukuruni Mwenyezi-Mungu!

10. “Tangazeni, enyi wapandapunda weupe,enyi mnaokalia mazulia ya fahari,nyinyi mnaotembea njiani, tangazeni jambo hilo.

11. Imbeni kupita wanamuziki kwenye visima vya maji,tangazeni ushindi wa Mwenyezi-Mungu,ushindi kwa wakulima wake katika Israeli.Ndipo watu wa Mwenyezi-Mungu waliposhuka malangoni.

12. “Amka, amka, Debora!Amka! Amka uimbe wimbo!Amka, Baraki mwana wa Abinoamu,uwachukue mateka wako.

13. Mashujaa waliobaki waliteremka,watu wa Mwenyezi-Mungu walikwenda kumpiganiadhidi ya wenye nguvu.

14. Kutoka Efraimu waliteremka bondeni,wakafuata ndugu zao watu wa Benyamini;kutoka Makiri walishuka makamanda,kutoka Zebuluni maofisa wakuu.

15. Wakuu wa Isakari wakafuatana na Debora,watu wa Isakari waaminifu kwa Baraki;wakamfuata mbio mpaka bondeni.Lakini miongoni mwa koo za Reubenikulikuwamo kusitasita kwingi.

Kusoma sura kamili Waamuzi 5