8. Walijichagulia miungu mipya,kukawa na vita katika nchi.Lakini hakukupatikana mwenye upanga au ngaokati ya watu 40,000 wa Israeli.
9. Nawapa heshima makamanda wa Israeliwaliojitoa kwa hiari yao kati ya watu.Mshukuruni Mwenyezi-Mungu!
10. “Tangazeni, enyi wapandapunda weupe,enyi mnaokalia mazulia ya fahari,nyinyi mnaotembea njiani, tangazeni jambo hilo.
11. Imbeni kupita wanamuziki kwenye visima vya maji,tangazeni ushindi wa Mwenyezi-Mungu,ushindi kwa wakulima wake katika Israeli.Ndipo watu wa Mwenyezi-Mungu waliposhuka malangoni.
12. “Amka, amka, Debora!Amka! Amka uimbe wimbo!Amka, Baraki mwana wa Abinoamu,uwachukue mateka wako.