Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:21-31 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mafuriko ya mto Kishoni yaliwachukua mbali,naam, mafuriko makali ya mto Kishoni.Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!

22. “Farasi walipita wakipiga shoti;,walikwenda shoti na kishindo cha kwato zao.

23. Malaika wa Mwenyezi-Mungu asema hivi:‘Uapizeni mji wa Merosi,waapizeni vikali wakazi wake;maana hawakuja kumsaidia Mwenyezi-Munguhawakumsaidia Mwenyezi-Mungu dhidi ya wenye nguvu’.

24. “Abarikiwe kuliko wanawake woteYaeli, mke wa Heberi, Mkeni.Naam, amebarikiwa kuliko wanawake wotewanaokaa mahemani.

25. Sisera alimwomba maji, naye akampa maziwa;alimletea siagi katika bakuli ya heshima.

26. Kwa mkono mmoja alishika kigingi cha hema,na kwa mkono wake wa kulia nyundo ya fundi;alimponda Sisera kichwa,alivunja na kupasuapasua paji lake.

27. Sisera aliinama, akaanguka;alilala kimya miguuni pake.Hapo alipoinama ndipo alipoanguka, amekufa!

28. “Mama yake Sisera alitazama dirishanialichungulia katika viunzi vyake, akalalamika:‘Kwa nini gari lake limechelewa?Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa kusikika?’

29. Jibu akalipata kwa wanawake wenye hekima:Akajituliza tena na tena kwa jibu hilo:

30. ‘Bila shaka wanatafuta na kugawana nyara;msichana mmoja au wawili kwa kila askari,vazi la sufu ya rangi kwa ajili ya Sisera.Vazi la sufu iliyotariziwa,na mikufu miwili ya nakshi kwa ajili ya shingo yangu!’

31. “Ee Mwenyezi-Mungu, waangamie adui zako wote!Lakini rafiki zako na wawe kama jua,wakati linapochomoza kwa mwanga mkubwa!”Nayo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arubaini.

Kusoma sura kamili Waamuzi 5