Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Kwa nini walibaki mazizini?Ili kusikiliza milio ya kondoo?Miongoni mwa koo za Reubenikulikuwamo kusitasita kwingi.

17. Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani.Kabila la Dani, kwa nini mlibaki merikebuni?Kabila la Asheri lilitulia huko pwani ya bahari,lilikaa bandarini mwake.

18. Watu wa Zebuluni ni watuwaliohatarisha maisha yao katika kifo.Hata wa Naftali walikikabili kifokwenye miinuko ya mashamba.

19. “Huko Taanaki, kando ya chemchemi za Megido,wafalme walikuja, wakapigana;wafalme wa Kanaani walipigana,lakini hawakupata nyara za fedha.

20. Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita,zilifuata njia zao, zilipigana na Sisera.

21. Mafuriko ya mto Kishoni yaliwachukua mbali,naam, mafuriko makali ya mto Kishoni.Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!

Kusoma sura kamili Waamuzi 5