Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 20:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Waisraeli, licha ya wa kabila la Benyamini, walikusanya watu 400,000 wawezao kutumia silaha. Wote walikuwa hodari wa vita.

18. Waisraeli wakaenda Betheli kutaka shauri kwa Mungu, wapate kujua kabila ambalo litakwenda kwanza kupigana na watu wa kabila la Benyamini. Mwenyezi-Mungu alitaja kabila la Yuda liende kwanza.

19. Basi, Waisraeli wakaenda asubuhi, wakapiga kambi yao karibu na mji wa Gibea.

20. Waisraeli wakatoka kupigana na watu wa kabila la Benyamini karibu na Gibea.

21. Watu wa kabila la Benyamini wakatoka nje ya mji wa Gibea wakapigana na Waisraeli, wakawaangusha chini siku hiyo, watu wa Israeli 22,000.

Kusoma sura kamili Waamuzi 20