Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 17:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Wakati huo kulikuwa na kijana mmoja Mlawi mjini Bethlehemu nchini Yuda.

8. Kijana huyo akaondoka Bethlehemu nchini Yuda, akaenda kutafuta mahali pengine pa kuishi. Katika safari yake akafika nyumbani kwa Mika katika nchi ya milima ya Efraimu.

9. Mika akamwuliza, “Umetoka wapi?” Naye akamjibu, “Mimi ni Mlawi, kutoka mjini Bethlehemu nchini Yuda. Nitakaa popote nitakapopata nafasi ya kukaa kama mgeni.”

10. Mika akamwambia, “Kaa pamoja nami, uwe kwangu kama baba na kuhani wangu. Nitakulipa vipande kumi vya fedha kila mwaka na mavazi pamoja na mahitaji yako.”

11. Huyo Mlawi akaingia akakubali, akakaa huko na kuwa kama mmoja wa wana wa Mika.

12. Naye Mika akamfanya kijana huyo Mlawi kuwa kuhani wake huko nyumbani kwake.

13. Kisha akasema, “Sasa najua kwamba Mwenyezi-Mungu atanifanikisha kwani nina kijana huyu Mlawi kama kuhani wangu.”

Kusoma sura kamili Waamuzi 17