Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 17:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Mika akamwambia, “Kaa pamoja nami, uwe kwangu kama baba na kuhani wangu. Nitakulipa vipande kumi vya fedha kila mwaka na mavazi pamoja na mahitaji yako.”

11. Huyo Mlawi akaingia akakubali, akakaa huko na kuwa kama mmoja wa wana wa Mika.

12. Naye Mika akamfanya kijana huyo Mlawi kuwa kuhani wake huko nyumbani kwake.

13. Kisha akasema, “Sasa najua kwamba Mwenyezi-Mungu atanifanikisha kwani nina kijana huyu Mlawi kama kuhani wangu.”

Kusoma sura kamili Waamuzi 17