Agano la Kale

Agano Jipya

Nehemia 9:34-38 Biblia Habari Njema (BHN)

34. Wafalme wetu, wakuu wetu,makuhani wetu na babu zetuhawajaishika sheria yakowala kujali amri yakona maonyo yako uliyowapa.

35. Hawakukutumikia katika ufalme wao,wala walipoyafurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi,katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapahawakuyaacha matendo yao maovu.

36. Na leo tumekuwa watumwa;tu watumwa katika nchi uliyowapa babu zetuwafurahie matunda na vipawa vyake vyema.

37. Kwa sababu ya dhambi zetu,utajiri wa nchi hiiunawaendea wafalme uliowaleta kututawala.Wanatutawala wapendavyohata na mifugo yetuwanaitendea wapendavyo,tumo katika dhiki kuu.”

38. Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara na wakuu wetu kwa maandishi; Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na mhuri wao.

Kusoma sura kamili Nehemia 9