Agano la Kale

Agano Jipya

Nahumu 3:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kushi ilikuwa nguvu yake;nayo Misri pia, tena bila kikomo;watu wa Puti na Libia waliusaidia!

10. Hata hivyo, ulichukuliwa mateka,watu wake wakapelekwa uhamishoni.Hata watoto wake walipondwapondwakatika pembe ya kila barabara;watu wake mashuhuri walinadiwa,wakuu wake wote walifungwa minyororo.

11. Ninewi, nawe pia utalewa;utamkimbia adui na kujaribu kujificha.

12. Ngome zako zote ni za tini za mwanzo;zikitikiswa zinamwangukia mlaji kinywani.

13. Tazama askari wako:Wao ni waoga kama wanawake.Milango ya nchi yako ni wazi mbele ya adui zako;moto umeyateketeza kabisa makomeo yake.

14. Tekeni maji muwe tayari kuzingirwa;imarisheni ngome zenu.Pondeni udongo kwa kuukanyagakanyaga,tayarisheni tanuri ya kuchomea matofali!

15. Lakini huko pia moto utawateketezeni,upanga utawakatilia mbali;utawamaliza kama nzige walavyo.Ongezekeni kama nzige,naam, ongezekeni kama panzi!

16. Wafanyabiashara wako waliongezeka kuliko nyota;lakini sasa wametoweka kama panzi warukavyo.

17. Wakuu wako ni kama panzi,maofisa wako kama kundi la nzige;wakati wa baridi wanakaa kwenye kuta,lakini jua lichomozapo, huruka,wala hakuna ajuaye walikokwenda.

Kusoma sura kamili Nahumu 3