9. Kushi ilikuwa nguvu yake;nayo Misri pia, tena bila kikomo;watu wa Puti na Libia waliusaidia!
10. Hata hivyo, ulichukuliwa mateka,watu wake wakapelekwa uhamishoni.Hata watoto wake walipondwapondwakatika pembe ya kila barabara;watu wake mashuhuri walinadiwa,wakuu wake wote walifungwa minyororo.
11. Ninewi, nawe pia utalewa;utamkimbia adui na kujaribu kujificha.
12. Ngome zako zote ni za tini za mwanzo;zikitikiswa zinamwangukia mlaji kinywani.
13. Tazama askari wako:Wao ni waoga kama wanawake.Milango ya nchi yako ni wazi mbele ya adui zako;moto umeyateketeza kabisa makomeo yake.
14. Tekeni maji muwe tayari kuzingirwa;imarisheni ngome zenu.Pondeni udongo kwa kuukanyagakanyaga,tayarisheni tanuri ya kuchomea matofali!
15. Lakini huko pia moto utawateketezeni,upanga utawakatilia mbali;utawamaliza kama nzige walavyo.Ongezekeni kama nzige,naam, ongezekeni kama panzi!
16. Wafanyabiashara wako waliongezeka kuliko nyota;lakini sasa wametoweka kama panzi warukavyo.
17. Wakuu wako ni kama panzi,maofisa wako kama kundi la nzige;wakati wa baridi wanakaa kwenye kuta,lakini jua lichomozapo, huruka,wala hakuna ajuaye walikokwenda.