Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3

Agano la Kale

Agano Jipya

Nahumu 3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wako mji wa mauaji!Umejaa udanganyifu mtupu na nyara tele,usiokoma kamwe kuteka nyara.

2. Sikia! Mlio wa mjeledi,mrindimo wa magurudumu,vishindo vya farasina ngurumo za magari!

3. Wapandafarasi wanashambulia,panga na mikuki inametameta;waliouawa hawana idadi,maiti wengi sana;watu wanajikwaa juu ya maiti!

4. Ninewi! Wewe umekuwa kama malaya.Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi,uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa umalaya wako,na watu wa mataifa kwa uchawi wako.

5. Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema nitapambana nawe;nitalipandisha vazi lako hadi kichwani,niyaache mataifa yauone uchi wako,tawala ziikodolee macho aibu yako.

6. Nitakutupia uchafu,na kukutendea kwa dharau,na kukufanya uwe kioja kwa watu.

7. Kisha wote watakaokuona watakukimbia wakisema,“Ninewi umeangamizwa,ni nani atakayeuombolezea?Nani atakayekufariji?”

8. Je, wewe Ninewi, ni bora kuliko Thebesi,mji uliojengwa kando ya mto Nili?Thebesi ulizungukwa na maji,bahari ilikuwa boma lake,maji yalikuwa ukuta wake!

9. Kushi ilikuwa nguvu yake;nayo Misri pia, tena bila kikomo;watu wa Puti na Libia waliusaidia!

10. Hata hivyo, ulichukuliwa mateka,watu wake wakapelekwa uhamishoni.Hata watoto wake walipondwapondwakatika pembe ya kila barabara;watu wake mashuhuri walinadiwa,wakuu wake wote walifungwa minyororo.

11. Ninewi, nawe pia utalewa;utamkimbia adui na kujaribu kujificha.

12. Ngome zako zote ni za tini za mwanzo;zikitikiswa zinamwangukia mlaji kinywani.

13. Tazama askari wako:Wao ni waoga kama wanawake.Milango ya nchi yako ni wazi mbele ya adui zako;moto umeyateketeza kabisa makomeo yake.

14. Tekeni maji muwe tayari kuzingirwa;imarisheni ngome zenu.Pondeni udongo kwa kuukanyagakanyaga,tayarisheni tanuri ya kuchomea matofali!

15. Lakini huko pia moto utawateketezeni,upanga utawakatilia mbali;utawamaliza kama nzige walavyo.Ongezekeni kama nzige,naam, ongezekeni kama panzi!

16. Wafanyabiashara wako waliongezeka kuliko nyota;lakini sasa wametoweka kama panzi warukavyo.

17. Wakuu wako ni kama panzi,maofisa wako kama kundi la nzige;wakati wa baridi wanakaa kwenye kuta,lakini jua lichomozapo, huruka,wala hakuna ajuaye walikokwenda.

18. Ewe mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala,waheshimiwa wako wamesinzia.Watu wako wametawanyika milimani,wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.

19. Hakuna wa kuyapa nafuu majeraha yako,vidonda vyako ni vya kifo.Wote wanaosikia habari zako wanashangilia.Maana ni nani aliyeuepa ukatili wako usio na kikomo?