Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 46:32-34 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Nitamweleza kwamba nyinyi ni wachungaji kwani mmekuwa mkichunga mifugo, na kwamba mmewasili pamoja na mbuzi, kondoo, ng'ombe na mali yenu yote.

33. Basi, Farao akiwaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’

34. Semeni: ‘Bwana, sisi watumishi wako, ni wafugaji wa mifugo tangu utoto wetu mpaka leo, kwani ndivyo walivyokuwa babu zetu’; semeni hivyo ili mruhusiwe kukaa katika eneo la Gosheni.” Yosefu alisema hivyo kwa sababu kwa Wamisri wachungaji wote wa kondoo ni chukizo.

Kusoma sura kamili Mwanzo 46