Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 46:16-29 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Gadi na wanawe: Sifioni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.

17. Asheri na wanawe: Imna, Ishva, Ishvi, Beria na Sera, dada yao. Beria na wanawe: Heberi na Malkieli.

18. Hawa kumi na sita ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Zilpa, mjakazi ambaye Labani alimpa Lea, binti yake.

19. Raheli alimzalia Yakobo wana wawili: Yosefu na Benyamini.

20. Huko Misri, Asenathi, binti Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efraimu.

21. Wana wa Benyamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.

22. Watu hao kumi na wanne ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Raheli, mkewe.

23. Dani na Hushimu, mwanawe.

24. Naftali na wanawe: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.

25. Hao saba ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Bilha, mjakazi ambaye Labani alimpa binti yake Raheli.

26. Jumla ya wazawa wa Yakobo aliokwenda nao Misri, bila kuwahesabu wake za wanawe, ilikuwa watu sitini na sita.

27. Huko nchini Misri Yosefu alikuwa amepata wana wawili. Kwa hiyo watu wote wa jamaa ya Yakobo walioingia Misri walikuwa sabini.

28. Yakobo akamtanguliza Yuda kwa Yosefu kumwomba waonane huko Gosheni; nao wakafika katika eneo la Gosheni.

29. Yosefu akapanda gari lake la farasi, akaenda kumlaki Israeli, baba yake, huko Gosheni. Alipomfikia baba yake, alimkumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.

Kusoma sura kamili Mwanzo 46