Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 3:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kisha akamwambia huyo mwanamume,“Kwa kuwa wewe umemsikiliza mkeo,ukala matunda ya mti ambayo nilikuamuru usile;kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi imelaaniwa.Kwa jasho utajipatia humo riziki yako,siku zote za maisha yako.

18. Ardhi itakuzalia michongoma na magugu,nawe itakubidi kula majani ya shambani.

19. Kwa jasho lako utajipatia chakulampaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa;maana wewe ni mavumbi, na mavumbini utarudi.”

20. Adamu akampa mkewe jina “Hawa”, kwani alikuwa mama wa binadamu wote.

21. Mwenyezi-Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.

Kusoma sura kamili Mwanzo 3