Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 10:6-20 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Watoto wa kiume wa Hamu walikuwa Kushi, Misri, Puti na Kanaani.

7. Watoto wa kiume wa Kushi walikuwa Seba, Hawila, Sabta, Raama na Sabteka. Watoto wa kiume wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.

8. Kushi alikuwa baba yake Nimrodi ambaye alikuwa shujaa wa kwanza duniani.

9. Alikuwa mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu, ndiyo maana kuna msemo usemao, “Kama Nimrodi mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu.”

10. Miji ya kwanza ya utawala wake ilikuwa Babuloni, Ereki na Akadi, katika nchi ya Shinari.

11. Kutoka huko, Nimrodi alikwenda Ashuru, akajenga miji ya Ninewi, Rehoboth-iri, Kala na

12. Reseni ulioko kati ya Ninewi na mji mkubwa wa Kala.

13. Misri alikuwa babu wa Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi,

14. Wapathrusi, Wakasluhi (ambao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.

15. Kanaani alikuwa babu yake Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,

16. na pia babu yao Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

17. Wahivi, Waarki, Wasini,

18. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye watu wa jamii mbalimbali za Kanaani walitawanyika,

19. hata eneo la nchi yao likawa toka Sidoni kuelekea kusini, hadi Gerari mpaka Gaza, na kuelekea mashariki hadi Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu hadi Lasha.

20. Hao ndio wazawa wa Hamu kadiri ya makabila yao, lugha zao, nchi zao na mataifa yao.

Kusoma sura kamili Mwanzo 10