Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 10:6-14 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Watoto wa kiume wa Hamu walikuwa Kushi, Misri, Puti na Kanaani.

7. Watoto wa kiume wa Kushi walikuwa Seba, Hawila, Sabta, Raama na Sabteka. Watoto wa kiume wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.

8. Kushi alikuwa baba yake Nimrodi ambaye alikuwa shujaa wa kwanza duniani.

9. Alikuwa mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu, ndiyo maana kuna msemo usemao, “Kama Nimrodi mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu.”

10. Miji ya kwanza ya utawala wake ilikuwa Babuloni, Ereki na Akadi, katika nchi ya Shinari.

11. Kutoka huko, Nimrodi alikwenda Ashuru, akajenga miji ya Ninewi, Rehoboth-iri, Kala na

12. Reseni ulioko kati ya Ninewi na mji mkubwa wa Kala.

13. Misri alikuwa babu wa Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi,

14. Wapathrusi, Wakasluhi (ambao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.

Kusoma sura kamili Mwanzo 10