Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 10:2-11 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Watoto wa kiume wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.

3. Watoto wa kiume wa Gomeri walikuwa Ashkenazi, Rifathi na Togama.

4. Watoto wa kiume wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu na Dodanimu.

5. Hawa ndio asili ya watu walioenea sehemu za pwani, kila watu kwa lugha yao, kwa jamaa zao na kufuata mataifa yao.

6. Watoto wa kiume wa Hamu walikuwa Kushi, Misri, Puti na Kanaani.

7. Watoto wa kiume wa Kushi walikuwa Seba, Hawila, Sabta, Raama na Sabteka. Watoto wa kiume wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.

8. Kushi alikuwa baba yake Nimrodi ambaye alikuwa shujaa wa kwanza duniani.

9. Alikuwa mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu, ndiyo maana kuna msemo usemao, “Kama Nimrodi mwindaji shujaa mbele ya Mwenyezi-Mungu.”

10. Miji ya kwanza ya utawala wake ilikuwa Babuloni, Ereki na Akadi, katika nchi ya Shinari.

11. Kutoka huko, Nimrodi alikwenda Ashuru, akajenga miji ya Ninewi, Rehoboth-iri, Kala na

Kusoma sura kamili Mwanzo 10