Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 10:16-32 Biblia Habari Njema (BHN)

16. na pia babu yao Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

17. Wahivi, Waarki, Wasini,

18. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye watu wa jamii mbalimbali za Kanaani walitawanyika,

19. hata eneo la nchi yao likawa toka Sidoni kuelekea kusini, hadi Gerari mpaka Gaza, na kuelekea mashariki hadi Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu hadi Lasha.

20. Hao ndio wazawa wa Hamu kadiri ya makabila yao, lugha zao, nchi zao na mataifa yao.

21. Shemu, mkubwa wa Yafethi, alikuwa baba yao Waebrania wote.

22. Watoto wa kiume wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.

23. Watoto wa kiume wa Aramu walikuwa Usi, Huli, Getheri na Mashi.

24. Arfaksadi alimzaa Shela, Shela akamzaa Eberi.

25. Eberi alikuwa na watoto wa kiume wawili; wa kwanza akamwita Pelegi kwa sababu wakati huo watu duniani waligawanyika, na wa pili akamwita Yoktani.

26. Yoktani alikuwa baba wa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

27. Hadoramu, Uzali, Dikla,

28. Obali, Abimaeli, Sheba,

29. Ofiri, Hawila na Yobabu. Hao wote walikuwa watoto wa Yoktani.

30. Nchi walimokaa ilienea toka Mesha mpaka Sefari katika nyanda za juu za mashariki.

31. Hao ndio wazawa wa Shemu, kadiri ya makabila yao, lugha zao, nchi zao na mataifa yao.

32. Hao ndio jamaa za watoto wa Noa, kadiri ya vizazi vyao na mataifa yao. Kutokana nao mataifa yote yalienea duniani baada ya gharika.

Kusoma sura kamili Mwanzo 10