Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 10:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Misri alikuwa babu wa Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi,

14. Wapathrusi, Wakasluhi (ambao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.

15. Kanaani alikuwa babu yake Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,

16. na pia babu yao Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

17. Wahivi, Waarki, Wasini,

18. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye watu wa jamii mbalimbali za Kanaani walitawanyika,

19. hata eneo la nchi yao likawa toka Sidoni kuelekea kusini, hadi Gerari mpaka Gaza, na kuelekea mashariki hadi Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu hadi Lasha.

Kusoma sura kamili Mwanzo 10