Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 6:8-16 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Mungu amekuonesha yaliyo mema, ewe mtu;anachotaka Mwenyezi-Mungu kwako ni hiki:Kutenda mambo ya haki,kupenda kuwa na huruma,na kuishi kwa unyenyekevu na Mungu wako.

9. Mwenyezi-Mungu anawaita wakazi wa mji,na ni jambo la busara sana kumcha yeye:“Sikilizeni, enyi watu wa Yuda;sikilizeni enyi mliokusanyika mjini.

10. “Je, nitavumilia maovuyaliyorundikwa nyumbani mwao,mali zilizopatikana kwa udanganyifu,na matumizi ya mizani danganyifu,jambo ambalo ni chukizo?

11. Je, naweza kusema hawana hatiawatu wanaotumia mizani ya danganyifuna mawe ya kupimia yasiyo halali?

12. Matajiri wa miji wamejaa dhuluma,wakazi wake husema uongo,kila wasemacho ni udanganyifu.

13. Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini,na kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.

14. Mtakula lakini hamtashiba;ndani mwenu njaa itazidi kuwauma.Mkiweka akiba haitahifadhiwa,na mkihifadhi kitu nitakiharibu kwa vita.

15. Mtapanda mbegu, lakini hamtavuna.Mtasindika zeituni, lakini hamtatumia hayo mafuta.Mtasindika zabibu, lakini hamtakunywa hiyo divai.

16. Nyinyi mnafuata mfano mbaya wa mfalme Omrina mfano wa jamaa ya mfalme Ahabuna mfano mbaya wa jamaa ya mwanawe, Ahabu,na mmefuata mashauri yao.Kwa hiyo nitawaleteeni maangamizi,na kila mtu atawadharau.Watu watawadhihaki kila mahali.”

Kusoma sura kamili Mika 6