Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 6:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Je, naweza kusema hawana hatiawatu wanaotumia mizani ya danganyifuna mawe ya kupimia yasiyo halali?

12. Matajiri wa miji wamejaa dhuluma,wakazi wake husema uongo,kila wasemacho ni udanganyifu.

13. Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini,na kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.

14. Mtakula lakini hamtashiba;ndani mwenu njaa itazidi kuwauma.Mkiweka akiba haitahifadhiwa,na mkihifadhi kitu nitakiharibu kwa vita.

15. Mtapanda mbegu, lakini hamtavuna.Mtasindika zeituni, lakini hamtatumia hayo mafuta.Mtasindika zabibu, lakini hamtakunywa hiyo divai.

16. Nyinyi mnafuata mfano mbaya wa mfalme Omrina mfano wa jamaa ya mfalme Ahabuna mfano mbaya wa jamaa ya mwanawe, Ahabu,na mmefuata mashauri yao.Kwa hiyo nitawaleteeni maangamizi,na kila mtu atawadharau.Watu watawadhihaki kila mahali.”

Kusoma sura kamili Mika 6