Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 5:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Nitaiharibu miji ya nchi yenu,na kuzibomolea mbali ngome zenu.

12. Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.

13. Nitaziharibu sanamu zenu,na nguzo zenu za ibada;nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.

14. Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,na kuiangamiza miji yenu.

15. Kwa hasira na ghadhabu yangu,nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”

Kusoma sura kamili Mika 5