11. Nitaiharibu miji ya nchi yenu,na kuzibomolea mbali ngome zenu.
12. Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.
13. Nitaziharibu sanamu zenu,na nguzo zenu za ibada;nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.
14. Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,na kuiangamiza miji yenu.
15. Kwa hasira na ghadhabu yangu,nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”