Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 5:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Jumuikeni mkajikusanye enyi watu wa Yerusalemu;mkisema: “Tumezingirwa, tumesongwa;naye kiongozi wa Israeli wanampiga shavuni kwa fimbo.”

2. Mwenyezi-Mungu asema,“Lakini wewe Bethlehemu katika Efratha,wewe ni mdogo tu kati ya jamii za Yuda,lakini kwako kutatoka mtawalaatakayetawala juu ya Israeli kwa niaba yangu.Asili yake ni ya zama za kale.”

3. Hivyo Mungu atawaacha watu wake kwa maadui,mpaka yule mama mjamzito atakapojifungua.Kisha ndugu zake waliobakia,watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.

4. Huyo mtawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Mwenyezi-Mungu,kwa fahari yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.Watu wake wataishi kwa usalama,maana atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.

Kusoma sura kamili Mika 5