Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 1:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza;nitatembea uchi na bila viatu.Nitaomboleza na kulia kama mbweha,nitasikitika na kulia kama mbuni.

9. Majeraha ya Samaria hayaponyeki,nayo yameipata pia Yuda;yamefikia lango la Yerusalemu,mahali wanapokaa watu wangu.

10. Msiitangaze habari hii huko Gathi,wala msilie machozi!Huko Beth-leafra mgaegae mavumbini kwa huzuni.

11. Nendeni enyi wakazi wa Shafiri,mkiwa uchi na wenye haya.Wakazi wa Zaanani msitoke nje ya mji wenu.Watu wa Beth-ezeli wanalia;msaada wao kwenu umeondolewa.

12. Wakazi wa Marothi wanangojea msaada kwa hamu kubwa,lakini maangamizi yaja kutoka kwa Mwenyezi-Mungukaribu kabisa na lango la Yerusalemu.

Kusoma sura kamili Mika 1