Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 8:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nani aliye kama mwenye hekima?Nani ajuaye hali halisi ya vitu?Hekima humletea mtu tabasamu,huubadilisha uso wake mwenye huzuni.

2. Tii amri ya mfalme, kwa sababu ya kiapo chako kitakatifu.

3. Usifanye haraka kuondoka mbele yake; wala usiwe na kiburi juu ya jambo baya, maana mfalme hufanya apendavyo.

4. Amri ya mfalme ni kauli ya mwisho; nani athubutuye kumwuliza, “Unafanya nini?”

5. Anayetii amri hatapata madhara, na mwenye hekima atajua kuna wakati na njia.

6. Naam, kila kitu kina wakati wake na njia yake, ingawa binadamu anakabiliwa na tatizo kubwa:

7. Hajui ni nini kitakachotukia baadaye, kwani nani awezaye kumjulisha yatakayotukia baadaye?

8. Hakuna mtu aliye na uwezo wa kushikilia roho yake asife; hakuna mtu aliye na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.

9. Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendwa hapa duniani, binadamu anapokuwa na uwezo wa kumkandamiza na kumdhuru binadamu mwenzake.

10. Tena, nimewaona waovu wakizikwa, na watu waliporudi kutoka mahali patakatifu wanawasifu humohumo mjini walimotenda maovu yao. Hayo nayo ni bure kabisa.

11. Kwa vile uovu haupatilizwi haraka, mioyo ya wanadamu hupania kutenda mabaya.

12. Wenye dhambi hutenda maovu mara mia, hata hivyo, huendelea kuishi. Walakini, mimi najua kwamba itakuwa heri kwao wamchao Mungu, kwa sababu ya uchaji wao;

Kusoma sura kamili Mhubiri 8