Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 7:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Afadhali kwenda kwenye matanga,kuliko kwenda kwenye karamu,kwa sababu walio hai yawapasa kukumbuka kwamba kifo chatungojea sisi sote.

3. Huzuni ni afadhali kuliko kichekomaana, huzuni ya uso ni faida ya moyo.

4. Moyo wa mwenye hekima huthamini matanga,lakini moyo wa mpumbavu hupenda raha.

5. Afadhali kusikia maonyo ya wenye hekimakuliko kusikiliza nyimbo za wapumbavu.

6. Maana, kicheko cha mpumbavuni kama mlio wa miiba motoni.Hayo nayo ni bure kabisa.

7. Mwenye hekima akimdhulumu mtu;hujifanya mwenyewe kuwa mpumbavukupokea rushwa hupotosha akili.

Kusoma sura kamili Mhubiri 7