Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 7:19-28 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Hekima humfanya mwenye busara kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi mjini.

20. Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.

21. Usitie maanani maneno yote wasemayo wanadamu, usije ukamsikia mtumishi wako akikutukana.

22. Wewe mwenyewe wajua moyoni kwamba umeapiza wengine mara nyingi.

23. Nimeyapima hayo yote kwa hekima; nikajisemea: “Nataka kuwa mwenye hekima!” Lakini hekima iko mbali sana nami.

24. Jinsi gani binadamu ataweza kugundua maana ya maisha; jambo hilo ni zito na gumu mno kwetu!

25. Hata hivyo, nilipania kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yaliyoko, na pia kujua uovu ni upuuzi, na upumbavu ni wazimu.

26. Jambo moja nililogundua lililo baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamke ambaye moyo wake ni mtego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayempendeza Mungu humkwepa mwanamke huyo, lakini mwenye dhambi hunaswa naye.

27. Haya, nakuambia mimi Mhubiri, ndio niliyogundua nilipofanya uchunguzi wangu kidogokidogo.

28. Nilipania kugundua mambo hayo tena na tena, lakini sikufaulu. Kati ya wanaume elfu moja, nilifaulu kumwona mwanamume mmoja, anayestahili heshima, lakini kati ya wanawake wote kama hao sikumwona hata mmoja anayestahili heshima.

Kusoma sura kamili Mhubiri 7