4. Tena niligundua kwamba juhudi zote za mtu na ujuzi wake katika kazi vyatokana na kuoneana wivu. Hayo nayo ni bure kabisa; ni sawa na kufukuza upepo.
5. Mpumbavu hafanyi kazina mwisho hujiua kwa njaa.
6. Ni afadhali kuwa na kidogo tu, pamoja na amani moyoni,kuliko kuwa na mengi, pamoja na taabu;sawa tu na kufukuza upepo.
7. Tena, niliona jambo moja bure kabisa duniani.
8. Nilimwona mtu mmoja asiye na mwana wala ndugu; hata hivyo, haachi kufanya kazi; hatosheki kamwe na mali yake; wala hatulii na kujiuliza: “Ninamfanyia nani kazi na kujinyima starehe?” Hilo nalo ni bure kabisa; ni shughuli inayosikitisha.
9. Ni afadhali kuwa wawili kuliko mtu kuwa peke yake. Kwa sababu wawili watapata tuzo la kazi yao.