Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 4:2-14 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Maana ninawapa maagizo mema,msiyakatae mafundisho yangu.

3. Mimi pia nilikuwa mtoto mwenye baba,nilikuwa mpole, kipenzi cha mama yangu.

4. Baba yangu alinifundisha hiki:“Zingatia kwa moyo maneno yangu,shika amri zangu nawe utaishi.

5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu;usisahau wala kupuuza maneno yangu.

6. Usimwache Hekima, naye atakutunza;umpende, naye atakulinda.

7. Jambo la msingi ni kujipatia hekima;toa vyote ulivyonavyo ujipatie akili.

8. Mthamini sana Hekima, naye atakutukuza;ukimshikilia atakupa heshima.

9. Atakuvika kilemba kizuri kichwani pako,atakupa taji maridadi.”

10. Mwanangu, sikia na kuyapokea maneno yangu,ili upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.

11. Nimekufundisha njia ya hekima,nimekuongoza katika njia nyofu.

12. Ukitembea hatua zako hazitazuiwa,wala ukikimbia hutajikwaa.

13. Zingatia mafundisho ya Hekima na usimwache aponyoke,mshike kwa makini maana yeye ni uhai wako.

14. Usijiingize katika njia ya waovu,wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.

Kusoma sura kamili Methali 4