Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 4:12-27 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Ukitembea hatua zako hazitazuiwa,wala ukikimbia hutajikwaa.

13. Zingatia mafundisho ya Hekima na usimwache aponyoke,mshike kwa makini maana yeye ni uhai wako.

14. Usijiingize katika njia ya waovu,wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.

15. Iepe njia hiyo wala usiikaribie;jiepushe nayo, uende zako.

16. Waovu kamwe hawalali wasipotenda uovu;hawapati usingizi wasipomkwaza mtu.

17. Maana uovu ndicho chakula chao,ukatili ndiyo divai yao.

18. Njia ya watu wema ni kama nuru ya alfajiri,ambayo hungaa zaidi na zaidi hata mchana kamili.

19. Lakini njia ya waovu ni kama giza nene,hawajui kinachowafanya wajikwae.

20. Mwanangu, sikiliza kwa makini maneno yangu,itegee sikio misemo yangu.

21. Usiyaache yatoweke machoni pako,yahifadhi ndani ya moyo wako.

22. Maana hayo ni uhai kwa mtu anayeyapata,ni dawa kwa mwili wake wote.

23. Linda moyo wako kwa uangalifu wote,maana humo zatoka chemchemi za uhai.

24. Tenga mbali nawe lugha potovu;wala midomo yako isitamke maneno madanganyifu.

25. Uyaelekeze macho yako mbele kwa ujasiri,mtazamo wako uwe mbele moja kwa moja.

26. Fikiria njia utakayochukua,na hatua zako zote zitakuwa kamili.

27. Usigeukie kulia wala kushoto;epusha mguu wako mbali na uovu.

Kusoma sura kamili Methali 4