23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.
24. Kuna viumbe vinne vidogo sana duniani,lakini vina akili sana:
25. Sisimizi: Wadudu wasio na nguvu,lakini hujihifadhia chakula wakati wa kiangazi;
26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;
27. nzige: Hawana mfalme,lakini wote huenda pamoja kwa vikosi;
28. mjusi: Waweza kumshika mkononi,lakini huingia katika ikulu.
29. Kuna viumbe vitatu vyenye mwendo wa kupendeza,naam, kuna viumbe vinne vyenye mwendo mzuri;
30. simba: Mnyama mwenye nguvu kuliko wote,wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;
31. jogoo aendaye kwa maringo;tena beberu;na mfalme mbele ya watu wake.
32. Kama umekuwa mpumbavu hata ukajisifu,au kama umekuwa unapanga maovu,chunga mdomo wako.
33. Maana ukisukasuka maziwa utapata siagi,ukimpiga mtu pua atatoka damu;kadhalika kuchochea hasira huleta ugomvi.