Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 30:14-29 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Kuna watu ambao meno yao ni kama upanga,na magego yao ni kama visu.Wako tayari kuwatafuna maskini wa nchi,na wanyonge walio miongoni mwa watu!

15. Mruba anao binti wawili wasemao, “Nipe, nipe!”Kuna vitu vitatu ambavyo kamwe havishibi,naam, vitu vinne visivyosema, “Imetosha!”

16. Kuzimu,tumbo la mwanamke lisilozaa,ardhi isiyoshiba maji,na moto usiosema, “Imetosha!”

17. Kama mtu akimdhihaki baba yake,na kudharau utii kwa mama yake,kunguru wa bondeni watamdonoa macho,na kuliwa na tai.

18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,naam, mambo manne nisiyoyaelewa:

19. Njia ya tai angani,njia ya nyoka mwambani,njia ya meli baharini,na kinachomvuta mwanamume kwa mwanamke.

20. Mwenendo wa mwanamke mwasherati ni hivi:Yeye hula, akajipangusa mdomo,na kusema, “Sijafanya kosa lolote!”

21. Kuna mambo matatu ambayo huitetemesha dunia,naam, mambo manne ambayo haiwezi kuyastahimili:

22. Mtumwa anayekuwa mfalme;mpumbavu anayeshiba chakula;

23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne vidogo sana duniani,lakini vina akili sana:

25. Sisimizi: Wadudu wasio na nguvu,lakini hujihifadhia chakula wakati wa kiangazi;

26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;

27. nzige: Hawana mfalme,lakini wote huenda pamoja kwa vikosi;

28. mjusi: Waweza kumshika mkononi,lakini huingia katika ikulu.

29. Kuna viumbe vitatu vyenye mwendo wa kupendeza,naam, kuna viumbe vinne vyenye mwendo mzuri;

Kusoma sura kamili Methali 30