14. Ukimtandika kiboko,utayaokoa maisha yake na kuzimu.
15. Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.
16. Moyo wangu utashangilia,mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.
17. Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.
18. Hakika kuna kesho ya milele,na tumaini lako halitakuwa bure.
19. Sikia mwanangu, uwe na hekima;fikiria sana jinsi unavyoishi.
20. Usiwe mmoja wa walevi wa divai,wala walafi wenye kupenda nyama,