Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 16:20-28 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Anayezingatia mafundisho atafanikiwa;heri mtu yule anayemtumainia Mwenyezi-Mungu.

21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.

22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.

23. Moyo wa mwenye hekima humwezesha kusema kwa busara;huyafanya maneno yake yawe ya kuvutia.

24. Maneno mazuri ni kama asali;ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.

25. Mtu aweza kuona njia yake kuwa sawa,lakini mwishowe humwongoza kwenye kifo.

26. Hamu ya chakula humhimiza mfanyakazi,maana njaa yake humsukuma aendelee.

27. Mtu mwovu hupanga uovu;maneno yake ni kama moto mkali.

28. Mtu mpotovu hueneza ugomvi,mfitini hutenganisha marafiki.

Kusoma sura kamili Methali 16