13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.
14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.
15. Uso wa mfalme ukingaa kuna uhai;wema wake ni kama wingu la masika.
16. Kupata hekima ni bora kuliko dhahabu;kupata akili ni chaguo bora kuliko fedha.
17. Njia ya wanyofu huepukana na uovu;anayechunga njia yake huhifadhi maisha yake.
18. Kiburi hutangulia maangamizi;majivuno hutangulia maanguko.
19. Afadhali kuwa mnyenyekevu na kuwa maskini,kuliko kugawana nyara na wenye kiburi.
20. Anayezingatia mafundisho atafanikiwa;heri mtu yule anayemtumainia Mwenyezi-Mungu.
21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.
22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.