Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 16:13-22 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.

14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.

15. Uso wa mfalme ukingaa kuna uhai;wema wake ni kama wingu la masika.

16. Kupata hekima ni bora kuliko dhahabu;kupata akili ni chaguo bora kuliko fedha.

17. Njia ya wanyofu huepukana na uovu;anayechunga njia yake huhifadhi maisha yake.

18. Kiburi hutangulia maangamizi;majivuno hutangulia maanguko.

19. Afadhali kuwa mnyenyekevu na kuwa maskini,kuliko kugawana nyara na wenye kiburi.

20. Anayezingatia mafundisho atafanikiwa;heri mtu yule anayemtumainia Mwenyezi-Mungu.

21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.

22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.

Kusoma sura kamili Methali 16