1. Binadamu hupanga mipango yake,lakini kauli ya mwisho ni yake Mwenyezi-Mungu.
2. Matendo ya mtu huonekana kwake kuwa sawa,lakini Mwenyezi-Mungu hupima nia ya mtu.
3. Mwekee Mwenyezi-Mungu kazi yako,nayo mipango yako itafanikiwa.
4. Mwenyezi-Mungu ameumba kila kitu kwa kusudi lake;hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.
5. Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;hakika mtu wa namna hiyo hataacha kuadhibiwa.
6. Kwa utii na uaminifu mtu huondolewa dhambi,kwa kumcha Mwenyezi-Mungu huepuka uovu.