Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 16:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Binadamu hupanga mipango yake,lakini kauli ya mwisho ni yake Mwenyezi-Mungu.

2. Matendo ya mtu huonekana kwake kuwa sawa,lakini Mwenyezi-Mungu hupima nia ya mtu.

3. Mwekee Mwenyezi-Mungu kazi yako,nayo mipango yako itafanikiwa.

4. Mwenyezi-Mungu ameumba kila kitu kwa kusudi lake;hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.

5. Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;hakika mtu wa namna hiyo hataacha kuadhibiwa.

6. Kwa utii na uaminifu mtu huondolewa dhambi,kwa kumcha Mwenyezi-Mungu huepuka uovu.

Kusoma sura kamili Methali 16