Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 11:7-21 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mwovu akifa tumaini lake nalo hutoweka;tazamio la asiyemcha Mungu huishia patupu.

8. Mtu mnyofu huokolewa katika shida,na mwovu huingia humo badala yake.

9. Asiyemcha Mungu huangamiza wengine kwa mdomo wake,lakini mwadilifu huokolewa kwa maarifa yake.

10. Waadilifu wakipata fanaka mji hushangilia,na waovu wakiangamia watu hupiga vigelegele.

11. Mji hufanikishwa kwa baraka za wanyofu,lakini huangamizwa kwa mdomo wa waovu.

12. Anayemdharau jirani yake hana akili,mtu mwenye busara hukaa kimya.

13. Apitapitaye akichongea hutoa siri,lakini anayeaminika rohoni huficha siri.

14. Pasipo na uongozi taifa huanguka,penye washauri wengi pana usalama.

15. Anayemdhamini mgeni atakuja juta,lakini anayechukia mambo ya dhamana yu salama.

16. Mwanamke mwema huheshimiwa,mwanamume mwenye bidii hutajirika.

17. Mtu mkarimu hufaidika yeye mwenyewe,lakini mtu mkatili hujiumiza mwenyewe.

18. Faida anayopata mwovu ni ya uongo,lakini atendaye mema hakika atapata faida ya kweli.

19. Mtu anayepania kuwa mwadilifu ataishi,lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.

20. Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini wenye mwenendo mwema ni furaha yake.

21. Hakika mwovu hataepa kuadhibiwa,lakini waadilifu wataokolewa.

Kusoma sura kamili Methali 11