Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 5:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Fahari tuliyojivunia imetokomea.Ole wetu kwa kuwa tumetenda dhambi!

17. Kwa ajili hiyo tumeugua moyoni,kwa mambo hayo macho yetu yamefifia.

18. Maana mlima Siyoni umeachwa tupu,mbweha wanazurura humo.

19. Lakini wewe Mwenyezi-Mungu watawala milele,utawala wako wadumu vizazi vyote.

20. Mbona umetuacha muda mrefu hivyo?Mbona umetutupa siku nyingi hivyo?

21. Uturekebishe ee Mwenyezi-Mungu, nasi tukurudie,uturudishie fahari yetu kama zamani.

22. Au, je, umetukataa kabisa?Je, umetukasirikia mno?

Kusoma sura kamili Maombolezo 5